Waimba, sikizeni,
Malaika mbinguni;
Wimbo wa tamu sana
Wa pendo zake Bwana;
"Duniani salama,
Kwa wakosa rehema."
Sisi sote na twimbe
Nao wale wajumbe;
Waimba, sikizeni,
Malaika mbinguni.
Ndiye Bwana wa mbingu,
Tangu milele Mungu,
Amezaliwa mwili,
Mwana wa mwanamwali;
Ametoka enzini
Kuja ulimwenguni
Mwokozi atufie,
Ili tusipotee,
Waimba, sikizeni,
Malaika mbinguni.
Seyidi wa amani
Ametoka Mbinguni,
Jua la haki, ndite
Atumulikiaye;
Amejivua enzi,
Alivyo na mapenzi,
Ataka kutuponya,
Kutuzalisha upya,
Waimba, sikizeni,
Malaika mbinguni.
Njoo upesi, Bwana,
Twakutamani sana;
Kaa nasi, Mwokosi,
Vita hatuviwezi;
Vunja kichwa cha nyoka,
Sura zako andika,
Tufanane na Wewe,
Kwetu sifa upewe,
Waimba, sikizeni,
Malaika mbinguni.
![]() Home |
Anthem |
Map |
Language |
History |
Culture |
People |
US Govt Info |
Sports |
Links |
Search |
©1996-2004 Timothy F. Bliss