Culture: Hymns


Luka 2:13 - Wingi wa jeshi la mbinguni.

WAIMBA SIKIZENI
Hark the Herald Angels

Waimba, sikizeni,
Malaika mbinguni;
Wimbo wa tamu sana
Wa pendo zake Bwana;
"Duniani salama,
Kwa wakosa rehema."
Sisi sote na twimbe
Nao wale wajumbe;
Waimba, sikizeni,
Malaika mbinguni.

Ndiye Bwana wa mbingu,
Tangu milele Mungu,
Amezaliwa mwili,
Mwana wa mwanamwali;
Ametoka enzini
Kuja ulimwenguni
Mwokozi atufie,
Ili tusipotee,
Waimba, sikizeni,
Malaika mbinguni.

Seyidi wa amani
Ametoka Mbinguni,
Jua la haki, ndite
Atumulikiaye;
Amejivua enzi,
Alivyo na mapenzi,
Ataka kutuponya,
Kutuzalisha upya,
Waimba, sikizeni,
Malaika mbinguni.

Njoo upesi, Bwana,
Twakutamani sana;
Kaa nasi, Mwokosi,
Vita hatuviwezi;
Vunja kichwa cha nyoka,
Sura zako andika,
Tufanane na Wewe,
Kwetu sifa upewe,
Waimba, sikizeni,
Malaika mbinguni.



Home

Anthem

Map

Language

History

Culture

People

US Govt Info

Sports

Links

Search

©1996-2004 Timothy F. Bliss