Kwa mfano wako, Mwokozi wangu,
Hiyo ni tumaini langu;
Mali za dunia nitatoa,
Nipate mfano kama Yesu.
Kwa mfano wako, Kwa mfano wako,
Ewe Mkombozi, niwe wako;
Unitilie muhuri yako,
Nigeuke kwa mfano wako.
Kwa mfano wako, Mwenye huruma,
Kusamehe na kuwa mwema;
Waangukao niwainue,
Wenye dhambi niwatafute.
Kwa mfano wako, Roho mpole,
Mtakatifu, Mvumilivu;
Kila kemeo kustahimili,
Mateso yote nikubali.
Kwa mfano wako, ninakujia,
Nipakwe na mafuta yako;
Nakuletea uzima wangu,
Tangu sasa na niwe wako.
Kwa mfano wako, ninakusihi,
Unimwagie Roho yako;
Niwe hekalu, ukae ndani,
Nistahilishe pendo lako.
![]() Home |
Anthem |
Map |
Language |
History |
Culture |
People |
US Govt Info |
Sports |
Links |
Search |
©1996-2004 Timothy F. Bliss