Mungu Baba yangu, U Mwaminifu,
Hakuna geuzo ndani yako;
Hubadiliki, wewe ndiwe sawa,
Jana, leo na siku zijazo.
Wewe Mwaminifu, Wewe Mwaminifu,
Kila siku fadhili napewa;
Vitu vyote ninavyo umenipa,
Wewe Mwaminifu kwangu Bwana.
Na viumbe vyote hulingamana,
Kuonyesha utukufu wako;
Jua, na mvua, mwezi tena nyota
Hulishuhudia pendo lako.
Samaha la dhambi, tena amani,
Hivi vyote ni baraka zako;
Nguvu zako zitadumu milele,
Nimebarikiwa sasa kwako.
![]() Home |
Anthem |
Map |
Language |
History |
Culture |
People |
US Govt Info |
Sports |
Links |
Search |
©1996-2004 Timothy F. Bliss