Mungu wangu, ndiye namwamini,
Po pote nilipo duniani;
Lo lote lanijialo,
Baba yangu hunitunza humo.
Namwamini Mungu hunipenda
Katika dhiki ama mashaka;
Matesoni hunilinda,
Baba yangu hunitunza sana.
Mungu hulinda viumbe vyake,
Huviongoza njiani mwake;
Najua anikumbuka,
Baba yangu hunitunza sana.
Njia ijapokuwa gizani,
Kondoo hawasahauliwi;
Mungu Mchunga aongoza
Baba yangu hunitunza sana.
![]() Home |
Anthem |
Map |
Language |
History |
Culture |
People |
US Govt Info |
Sports |
Links |
Search |
©1996-2004 Timothy F. Bliss